Friday, May 31, 2013

Zifahamu sababu za ugumbwa kwa wanaume



Ukosefu wa nguvu za kiume nchini twaweza kusema  ni janga. Hii ni kutokana na tafiti zilizowahi kufanywa na pia kuzagaa kwa vibao vya matangazo kuhusu dawa au tiba ya tatizo hilo.
Tatizo hili halipo kwa wazee kama ilivyodhaniwa zamani, bali hata kwa vijana, wake kwa waume wamekuwa wakiguswa na tatizo hilo.

Sababu nyingi zimewahi kuanishwa kuchochea ugumba kwa wanaume ikiwamo maradhi, kutazama luninga kwa muda mrefu na kutofanya mazoezi.

Hivi karibuni wataalamu katika Jarida la Jinsia na Tiba  la nchini Uingereza, lililochapishwa Januari lilieleza sababu kuu duniani zinazochochea ugumba kwa wanaume iwe wa muda mrefu au wa kudumu.

Taasisi ya Taifa ya Afya ya nchini Marekani (NIH) inaeleza kwamba sababu za jumla za ugumba ni umri na  asilimia nne ya wanaume wenye umri wa miaka 50  na kuendelea wanaweza kuwa na tatizo hilo wakati nusu ya wanaume wenye umri wa miaka 75 wanakumbwa na ugumba.

Daktari wa Upasuaji na Nguvu za Kiume katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Maryland,  Dk Andrew Kramer anasema karibu nusu ya wanawake na wanaume wote duniani wanakosa nguvu za kiume aidha moja kwa moja au katika nyakati fulani za maisha yao.

Madereva
Dk Kava anasema wakati wa zama za chuma ilibainika kwamba wanaume wanaoendesha baiskeli kwa muda mrefu, waendesha farasi na madereva wa magari kwa muda mrefu wamo hatarini kukosa nguvu za kiume.

Jarida la tiba lilifanya utafiti na kubaini kuwa asilimia nne ya wanaume wanaoendesha baiskeli kwa saa tatu au zaidi kwa wiki wanapata matatizo ya nguvu za kiume.

Anasema unapokaa kwenye gari, farasi au baiskeli kwa muda mmrefu unaweka nguvu katika neva na mishipa midogo inayobeba damu kwenda katika uume.

Anafafanua kwamba uendeshaji wa vyombo hivyo kwa muda mrefu unaharibu mishipa midogo na damu haiendi inavyotakiwa katika uume.

CHANZO: GAZETI MWANANCHI

No comments:

Post a Comment