Friday, May 31, 2013

The 7 Unconventional Ways Of Thinking

1. “Welcome the pain”


Yep! Welcome the pain. Accept it willingly.
There’s a saying, “Pain is weakness leaving the body”, which means to say, no matter how tough or how much pain you’re feeling, you’re going to emerge stronger after that. So don’t be afraid when things get tough. Push yourself to accept what is coming instead and know that you’re going to grow from it.

2. “Look forward to feeling good”


This is my main, personal method in motivating myself. I believe that when you work hard, the feeling you get after that is the reward. The sense of satisfaction and accomplishment is the backbone of it all.
The fitness mantra, “Do you want to be sore, or sorry later?” works the same way.
So only aim for the feeling. Ask yourself how you want to feel later only. Forget about how you’d feel in between.

3. “Stop moving forward, take a step back instead”


Stop progressing altogether for a second. Just stop.
Take a step back instead.
It may seem paradoxical, but you know what it can do for you? You’ll be able to gain more clarity.
Go back for a second, re-evaluate your goals and remember your why. This effectively gives you the motivation to move forward.
And you’ll make better progress.

4. “Quit”


Or better yet, quit. Give up altogether on what you’re doing.
This requires some reflection and evaluation though. Sometimes quitting is the best thing you can do. You just have to realize that what you’re doing isn’t helping you anymore.
And after you quit, you’re free to do whatever you want as you’re no longer trapped by whatever it is which held you down.

5. ”Have a really good break”


This kind of goes hand in hand with point (2): Look forward to feeling good.
I find that a lot of people have lousy breaks. They don’t do themselves the favour they deserve. E.g. Instead of recognizing that a break time is a time to recharge, they end up being completely idle by doing mindless things like surfing Facebook, Twitter or watching random YouTube videos they aren’t even interested in watching in the first place. That is dead time. It does not help you at all and before you know it, you’re back to work.

6. “Failure is your best friend”


Or, failure is your ally.
Embrace failure, for it will give you the best and most meaningful lessons you actually need to move forward. That being said, failure is not the end.
When you don’t get the results you want, it doesn’t mean it’s over. Instead, you’re given the opportunity to learn and grow the fastest way possible.

7. ”Have fun”


Whatever it is in life, just have fun. Make that your sole aim.
Don’t take life so seriously. Laugh at your mistakes. Never sweat the small stuff. Just have fun, and be thankful for what you have, and that everything is going to be okay anyway.

Hoja ya ushoga yatikisa Bunge

Mbunge wa Nyamagana(Chadema), ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ezekia Wenje, akitolewa nje ya Ukumbi wa Bunge na askari wa Bunge huku akionyesha alama ya ‘V’, baada ya wabunge wa CUF kutaka kumpiga, kutokana na hotuba yake waliyodai kuwaudhi wabunge hao. Picha na Emmanuel Herman. 


















Dodoma.

 Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai ameahirisha mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, baada ya msemaji wa kambi ya upinzani kwa wizara hiyo kukataa kuomba radhi kulingana na maagizo ya kiti cha Spika.

Ndugai alikuwa amemwamuru msemaji huyo wa Upinzani, Ezekiah Wenje aombe radhi kwa kile alichoeleza ni kukashifu chama cha CUF na afute maneno ya kashfa hizo kwenye hotuba yake.

Wenje alikubali kutosoma maneno hayo yaliyokuwa kwenye hotuba hiyo lakini akakataa kuomba radhi kwa maelezo kuwa yaliyoandikwa ni ya ukweli na ana ushahidi.

Awali wakati wa asubuhi pia Ndugai alilazimika kuahirisha kikao cha Bunge, baada ya kuzuka vurugu kubwa kati ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (CUF).

Vurugu hizo zilizuka baada ya Mbunge wa CUF (Mtambile) Masoud Salim, kutoa hoja ya kutaka Msemaji wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekiel Wenje, kusitisha hotuba yake kwa kile alichoeleza kuwa “imejaa uzushi, uhuni, uzandiki, uongo na ushenzi.”
Salim alitoa hoja hiyo saa 6:15 mchana, wakati Wenje akiwa anasoma hotuba hiyo katika ukurasa wa tatu.
“Mwongozo wa Spika,” alisema Salim muda mfupi kabla Naibu Spika Ndugai, hajampa fursa ya kutoa hoja yake.

Salim aliendelea: “Natoa hoja kwamba hotuba hii ni ya kizushi. Huu ni uhuni, uongo, ushenzi na uzandiki. Siyo ya kusomwa bungeni.”

Alitoa kauli hiyo akinukuu maneno yaliyoko kwenye ukurasa wa 8 wa kitabu cha hotuba hiyo yanayoeleza kuwa,”...Kwa upande wa CUF, kutokana na itikadi zake za mrengo wa kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake mikuu ni pamoja na kupigania haki za ndoa ya jinsia moja, usagaji na ushoga…’

Kipengele kilichowaudhi CUF kilisema hivi: “Hii ni kwa mujibu wa tangazo lao (CUF) kwenye mtandao wao wa umoja wa maliberali ulimwenguni, likiungwa mkono na Waziri wa Haki na Usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone kutoka chama cha Liberal Democrats wakati chama hicho kilipokuwa kinapitisha azimio la kuruhusu ndoa za jinsia moja kama haki ya mtu mmoja mmoja.

Salim alikiomba kiti cha Spika, kuamrisha Chadema waombe radhi, wafute kauli hiyo na Kamati ya Maadili iifanyie kazi taarifa yao kwa kuwa si ya kistaarabu.

“Kwanza wakome, wakome kwa asilimia 100. Wahuni hawa na tunataka wachukuliwe hatua za kinidhamu,” alisema Salim, huku akishangiliwa na Mbunge wa Nkasi (CCM), Ali Kessy ambaye aliibuka kitini na kuitikia,” Apigwe, apigwe, Msagaji mwenyewe (Wenje).”

CHANZO: GAZETI MWANANCHI


Zifahamu sababu za ugumbwa kwa wanaume



Ukosefu wa nguvu za kiume nchini twaweza kusema  ni janga. Hii ni kutokana na tafiti zilizowahi kufanywa na pia kuzagaa kwa vibao vya matangazo kuhusu dawa au tiba ya tatizo hilo.
Tatizo hili halipo kwa wazee kama ilivyodhaniwa zamani, bali hata kwa vijana, wake kwa waume wamekuwa wakiguswa na tatizo hilo.

Sababu nyingi zimewahi kuanishwa kuchochea ugumba kwa wanaume ikiwamo maradhi, kutazama luninga kwa muda mrefu na kutofanya mazoezi.

Hivi karibuni wataalamu katika Jarida la Jinsia na Tiba  la nchini Uingereza, lililochapishwa Januari lilieleza sababu kuu duniani zinazochochea ugumba kwa wanaume iwe wa muda mrefu au wa kudumu.

Taasisi ya Taifa ya Afya ya nchini Marekani (NIH) inaeleza kwamba sababu za jumla za ugumba ni umri na  asilimia nne ya wanaume wenye umri wa miaka 50  na kuendelea wanaweza kuwa na tatizo hilo wakati nusu ya wanaume wenye umri wa miaka 75 wanakumbwa na ugumba.

Daktari wa Upasuaji na Nguvu za Kiume katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Maryland,  Dk Andrew Kramer anasema karibu nusu ya wanawake na wanaume wote duniani wanakosa nguvu za kiume aidha moja kwa moja au katika nyakati fulani za maisha yao.

Madereva
Dk Kava anasema wakati wa zama za chuma ilibainika kwamba wanaume wanaoendesha baiskeli kwa muda mrefu, waendesha farasi na madereva wa magari kwa muda mrefu wamo hatarini kukosa nguvu za kiume.

Jarida la tiba lilifanya utafiti na kubaini kuwa asilimia nne ya wanaume wanaoendesha baiskeli kwa saa tatu au zaidi kwa wiki wanapata matatizo ya nguvu za kiume.

Anasema unapokaa kwenye gari, farasi au baiskeli kwa muda mmrefu unaweka nguvu katika neva na mishipa midogo inayobeba damu kwenda katika uume.

Anafafanua kwamba uendeshaji wa vyombo hivyo kwa muda mrefu unaharibu mishipa midogo na damu haiendi inavyotakiwa katika uume.

CHANZO: GAZETI MWANANCHI

Dawa za ARV zauzwa mitaani huko Rorya

Rorya. 

Imebainika kuwa dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa Ukimwi (ARVs) zinazotolewa katika Hospitali ya Wilaya ya Rorya mkoani Mara, zimezagaa mitaani kwa kuuzwa kwenye maduka binafsi na yanayomilikiwa na watumishi wa vituo vya afya vya Serikali.


Akizungumnza katika kikao cha Baraza la Madiwani wilayani Rorya, Diwani wa Kata ya Mirare, Peter Ayoyi (CCM), alisema uzagaaji wa dawa hizo ulibainika baada ya halmashauri kufanya msako wa dawa za Serikali katika maduka binafsi ya kuuza dawa wilayani humo.

“Inasikitisha kuwa dawa za hospitali zinauzwa kwenye maduka binafsi hata wagonjwa wa Ukimwi wananunua dawa za kurefusha maisha kwenye maduka hayo, Naomba kujua? Inakuwaje dawa za Hospitali za Serikali zinauzwa au zinapatikana katika maduka ya mitaani?,” alihoji Ayoyi.


Akijibu swali la Ayoyi, Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji ambaye ni Diwani wa Kata ya Koryo, Peter Sarungi (CCM) alikiri kuwa ni kweli dawa za hospitali zikiwamo za kurefusha maisha zinauzwa katika maduka ya dawa yanayomilikiwa na watu binafsi.

Diwani Peter Ayoyi alimtaka Mganga Mkuu, Daniel Chacha na halmashauri ya wilaya kuwachukulia hatua za kisheria wamiliki wa maduka yaliyokutwa yakiuza dawa za Serikali na za kurefusha maisha, kwa kuwa tangu ukaguzi huo ufanyike bado watu hao hawajachukuliwa hatua. 
   

Wenye divisheni ziro 30,000 wapeta

Dar es Salaam

Wanafunzi 30,063 waliopata daraja sifuri katika matokeo yaliyopita, wameula baada ya kupandishwa hadi daraja la nne kutokana na ukokotoaji upya wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyofanywa na Baraza la Mitihani la Taifa (Nacte) na kutangazwa jana.
Marekebisho hayo yalifanyika baada ya kufutwa kwa matokeo ya awali yaliyotangazwa Februari 18, mwaka huu.

Kufutwa kwa matokeo hayo, ilikuwa ni utekelezaji wa sehemu ya mapendekezo ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, baada ya wanafunzi 240,909 kupata daraja sifuri kwenye matokeo yaliyotangazwa mara ya kwanza.

Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema sasa watakaokuwa na sifuri ni 210,846 sawa na asilimia 56.92 wakati wavulana wakiwa ni 104,259 na wasichana 106,587.
Hiyo ina maana kuwa sasa ufaulu umepanda na kuwa asilimia 43.08 badala ya ule wa kwanza ambao ulikuwa asilimia 34.5.

Dk Kawambwa alisema kutokana na ukokotoaji mpya wa matokeo ya sasa, idadi ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo kwa daraja la kwanza mpaka la nne imeongezeka na kufikia wanafunzi 159,747 kutoka 126,847.

Wanafunzi waliopata daraja la kwanza ni 3,242 wavulana wakiwa ni 2,179 na wasichana 1,063 ikiwa ni asilimia 0.88 ya matokeo yote, daraja la pili ni 10,355 sawa na asilimia 2.8 wavulana wakiwa 7,267 na wasichana 3,088.

Waliopata daraja la tatu ni 21,752 sawa na asilimia 5.87 wavulana wakiwa 14,979 na wasichana 6,773, daraja la nne ni 124,260 sawa na asilimia 33.54 .

Tofauti na matokeo yaliyofutwa, ambayo watahiniwa waliopata daraja la kwanza walikuwa ni 1,641, wavulana wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456 na wasichana 1997.


Waliopata daraja la tatu walikuwa 15,426, wavulana 10,813 na wasichana 4,613, waliopata daraja la nne 103,327, wavulana 64,344 na wasichana 38,983 huku waliopata sifuri wakiwa 240,903, wavulana 120,664 na wasichana 120,239.

Dk Kawambwa alieleza watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani huo walikuwa ni 480,029 na waliofanya ni 458,139 sawa na asilimia 95.44.

Alisema kuwa watahiniwa wa shule waliosajiliwa kufanya mtihani huo walikuwa ni 411,225 na waliofanya ni 397,138 sawa na asilimia 96.57 huku wa kujitegemea wakiwa ni 68,804 na waliofanya ni 61,001.

Wednesday, November 21, 2012


UTAFITI umebaini kuwa sindano za uzazi wa mpango zinachangia kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kuwa zina vichocheo vingi ambavyo vinahuisha virusi vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

Inaelezwa kuwa walio katika hatari zaidi ya maambukizi hayo ni wanawake walioko katika ndoa kwa kuwa ndiyo wanaotumia zaidi sindano hizo.

Utafiti huo uliofanywa na wanasayansi wa Marekani na kuripotiwa na gazeti la The Guardian la Uingereza, umebaini kuwa wanawake wanaotumia sindano za uzazi wa mpango wapo katika hatari mara mbili ya kupata maambukizi ya Ukimwi au kuwaambukiza wenzi wao, kuliko wengine.

Katika utafiti huo uliofanywa katika nchi saba zinazoendelea barani Afrika ikiwamo Tanzania, wanasayansi hao kutoka Chuo Kikuu cha Washington, walipendekeza ushauri zaidi utolewe kwa wanandoa kabla mtu hajajiingiza kwenye matumizi ya sindano kama njia ya kupanga uzazi.

Utafiti huo ulifanyika kwa wanandoa 3,790 kutoka nchi za Tanzania, Afrika Kusini, Zimbabwe, Uganda, Kenya, Rwanda na Botswana, ulichapishwa kwa mara ya kwanza katika Jarida la Afya la Lancet kabla ya kunukuliwa na gazeti la The Guardian.

Utafiti umebaini pia kuwa zaidi ya wanawake 140 milioni duniani wanatumia njia mbalimbali za uzazi wa mpango, huku wanandoa wengi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, wanaoishi na VVU wakichagua kutumia sindano kama njia ya kuzuia mimba zisizotarajiwa.

Wanasayansi hao walikusanya taarifa kati ya wanandoa 3,790 ambao mmoja wao anaishi na VVU na mwenza wake akiwa hana maambukizo.

Aidha, wanawake ambao wanaishi na VVU na wanatumia sindano hizo pia walikuwa katika hatari zaidi ya kuwaambukiza wenzi wao.

Vipimo vilionyesha kuwa sindano hizo ambazo zina vichocheo ambavyo vinavipa nguvu virusi ndani ya nyumba ya uzazi (cervix).

Imeelezwa kuwa njia za uzazi wa mpango zinazohamasishwa zaidi na kupendwa zaidi na wanawake ni sindano, ambazo wanawake wanasema kuwa zinadumu kwa muda mrefu na zinaweza kutumika bila ya ruhusa au mume kufahamu.

Kiongozi mkuu wa utafiti huo, Renee Heffron wa Chuo Kikuu cha Washington alisema sindano za uzazi wa mpango zina vichocheo vingi ambavyo huvihuisha vijidudu vya Ukimwi katika nyumba ya uzazi na kuvipa nguvu ya kusambaa.

 “Ni vyema sasa kama tutasisitiza njia za uzazi wa mpango ambazo ni salama zaidi kama vile mipira ya kiume au njia nyingine ambazo hazina vichocheo (hormones) au zina kiasi kidogo cha vichocheo,” alisema Dk Heffron.

Mwanasayansi mwingine, Charles Morrison wa Kituo cha Afya cha Durham, nchini Marekani alisema uhamasishaji wa matumizi ya sindano za uzazi wa mpango unachochea maambukizi zaidi katika nchi za Jangwa la Sahara.

“Ushauri wangu kwa nchi zinazoendelea ni kuacha matumizi ya njia za uzazi wa mpango zenye vichocheo, ili tupunguze maambukizi, jibu la tatizo hili linatakiwa litafutwe sasa, nchi zinazohusika zinatakiwa zishiriki katika hili,” alisema.

Alivitaka vituo vya afya vitoe ushauri kwa wanawake kutumia kondomu badala ya sindano au vidonge.

Mara nyingi watu wanaotumia vidonge, wengi si wanandoa, mtu anayemeza vidonge vya kuzuia mimba anaogopa zaidi mimba, si Ukimwi.

Huchoche hamu ya mapenzi

Mfamasia katika Kitengo cha Dawa kwa watu wanaoishina VVU katika Hospitali ya Amana, Christopher Masika alisema anaafiki kuwa sindano na hata vidonge vinaweza kuwa ni sababu inayochochea maambukizi kwa sababu ya uhuru.

“Ninachokiona mimi katika hilo ni uhuru. Mtu anapotumia sindano huwa huru kufanya ngono kwa kuwa hana hofu ya mimba, hicho kinaweza kumfanya apate maambukizi kwa urahisi, tofauti na anapotumia kondomu,” alisema.

Alisema wapo baadhi ambao wakitumia sindano hizo vichocheo vinawafanya wapate hamu zaidi ya kufanya mapenzi, hivyo huanza kutembea na wanaume wengine.

Aliongeza kuwa mtu anayeishi na VVU akizuia mimba kwa njia ya sindano, ni rahisi kupata maambukizi mapya kutoka kwa mwenza wake.

Masika alisema wanawake wapewe elimu zaidi kwani wapo ambao wanadanganywa kuwa njia za uzazi wa mpango kama sindano, povu zinaweza kuzuia maambukizi, jambo ambalo si la kweli.

Wakati huohuo baadhi ya wanandoa wanaoishi na VVU wanaopata matibabu katika Hospitali ya Amana wamesema kuwa tangu waanze kutumia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) hamu ya kufanya mapenzi imeongezeka kwa kasi kubwa.

Mkuu wa Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (Tacaids), Dk Arodia Mulokozi, alisema taasisi yake haiwezi kuzungumza lolote kuhusu utafiti huo, badala yake alilitaka Mwananchi kuzungumza na Kitengo cha Afya ya Uzazi wa Mpango cha Muhimbili.

“Hatuhusiki na masuala ya uzazi wa mpango, nafikiri unaweza kuzungumza na Kitengo cha ‘Reproductive Health’ cha Muhimbili,” alisema Dk Mulokozi.

Waziri wa Afya hakupatika, lakini msemaji wa wizara hiyo, Nsachris Mwamwaja alisema ni mapema mno kuchangia kuhusu utafiti huo, atafanya hivyo pindi atakapopata taarifa zaidi.

Mratibu wa Mpango wa  Uzazi wa Mpango Tanzania (Umati), Dk Morris Hiza amekiri kuufahamu utafiti huo, lakini akaeleza kuwa haujajitosheleza na bado una maswali mengi.

“Nilikuwapo wakati Heffron anawasilisha utafiti wake mjini Geneva, lakini nakumbuka mkutano ule wa WHO (Shirika la Afya Duniani) uliukataa,” alisema.

Alieleza kuwa Heffton alifanya utafiti huo kwa nyani na wanawake makahaba pekee.


CHANZO: MWANANCHI

Wednesday, October 31, 2012

Bomu laua watoto watano

Watoto watano wamekufa baada ya kulipukiwa na bomu la kutupa kwa mkono walilookota wakati wakikusanya vyuma chakavu wilayani Karagwe Mkoa wa  Kagera.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Philip Kalangi, alithibitisha kutokea tukio hilo jana asubuhi katika Kijiji cha Rugarama Kata ya Iyande wilayani humo wakati wakichezea bomu hilo nyumbani ambalo liliokotwa juzi na Evadius Robert (17) akidhani kilikuwa chuma chakavu.


Aliwataja watoto  kuwa ni Fenias Frank (3);  Faraji Frank (1); Edgar Gidion (15); Faustin Alfonce (17) na Patric Kamali (12).


Alisema watalaam wa mabomu wa Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walifika eneo hilo kufanya uchunguzi  ili kubaini bomu hilo lilitoka wapi hadi kufika hapo.


Aliwataka wakazi wa eneo hilo kuacha kuokota kitu wasichokijua ambacho kinachofanana na chuma ili kuepuka majanga ya kulipukiwa na mabomu kama yamebakia sehemu hizo.


TAARIFA ZA AWALI


Taarifa za awali kabla Kamanda Kalangi kuzungumza na NIPASHE jana jioni, zilieleza kuwa watu saba wakiwamo wanne wa familia moja, wakazi wa kijiji hicho wamekufa kwa kulipukiwa na  bomu.


Taarifa hizo kutoka wilayani Karagwe zilieleza kuwa tukio hilo lilitokea jana  saa nne asubuhi kijijini hapo na kusababisha vifo vya watu saba wakiwa watoto chini ya miaka 18.

 Waliotajwa kufa o ni  Eladius Robert (15), Fenius Frank (3), Faraja Frank (1), Scatus Kamali (15), Nelson Alphonce (14), Edger Gidion (14) na mmoja ambaye jina lake halikufahamkika, lakini alikadiriwa kuwa na umri wa miaka 17.

Imeelezwa kuwa watoto hao walikuwa katika shughuli ya kuokota vyuma chakavu katika kijiji hicho kwa ajili ya kuuza kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na ununuzi wa vyuma chakavu wilayani humo.


Mmoja wa wazazi wa watoto hao, Frank Robert (35),  mkazi wa kijiji hicho, aliwaambia waandishi wa habari kuwa watoto hao walionekana asubuhi wakiokota vyuma chakavu kwa ajili ya kuuza na kuwa ghafla alisikia mlipuko wa kishindo ambao ulisababisha vifo vyao.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, Luteni Kanali  Benedict Kitenga, alithibitisha kutokea kwa vifo hivyo  ambavyo vinadaiwa kusababishwa na bomu la kutupwa kwa mkono.


Kitenga  aliwataka wakazi wa wilaya za Karagwe na Kyerwa hususani zile zinazopakana na nchi jirani kuwa waangalifu.

WAWILI WAFA, 20 WAJERUHIWA


Watu wawili wamefariki papo hapo na wengine 20 kujeruhiwa vibaya katika ajali ya lori aina ya Canter walilokuwa wakisafiri  kutoka Muheza mjini kuelekea Tarafa ya Amani, mkoani Tanga.


Ajali hiyo ilitokea jana  jioni katika maeneo ya Daraja Mbili  kijiji cha Ubembe, Kata ya Nkumba wilayani Muheza na kuthibitishwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Tanga, Jafari Mohamed.


Inadaiwa kuwa Canter hilo lenye namba za usajili T 497 ATU lilipata ajali hiyo wakati likiwa limebeba zaidi ya watu 30 na mizigo.


Waliokufa ni  Omari Salim, mkazi wa Kazita Amani na Renard Yusuph (7). Miili yao imehifadhiwa chumba cha maiti cha Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza.


Waliojeruhiwa ni Zena Kasimu; Zuena Husseni; Mele Yohana; Salimu Luka; Mariam Mchongoma; Moza Omari; Rehema Omari; Happy Mkai; Mathayo Kusaga; Sadiki Omari; Emanuel Bakari na Godfrey Pesambili.


Wengine ni Chedi Hassan; Omari Juma; Joseph Logasila; Ibarahimu Rashidi;  Ramadhani Ally; Ally Abdallah; Ramadhani Athumani na Ibarahim Makame.


Kundi la watu jana jioni walifurika katika hospitali hiyo kuwatafuta ndugu zao ambao walikuwa wakisafiri kwa lori hilo huku vilio vikitawala.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Ibrahim Matovu; Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Amiri Kiroboto; Mkuu wa Wilaya hiyo, Subira Mgalu na madiwani walifika hospitalini hapo kuwajulia hali majeruhi hao na kuwapa pole
.






CHANZO: NIPASHE